This archive report was first published on 24 July 2019.
Kituo cha habari Tuko liliripoti kuwa mchungaji wa kanisa wa Maiani, Makueni, alikataa kubariki sadaka baada ya kuona kwamba ilikuwa kidogo na haingekuwa na uwezo wa kutosheleza mahitaji yake ya kibinafsi.
Alipokuwa akilalamika kila Jumapili, mchungaji huyo alikuwa akisema kwamba sadaka ilikuwa ni duni mno na kuwataka waumini wake kuongeza mkono.
Alipokuwa akikubali sadaka, alitupa jicho ndani ya kapu la sadaka na kisha akatikisa kichwa ishara kwamba hakuridhishwa na alichokiona.
Alisema hangeibariki kwa kuwa ilikuwa kidogo na haingekuwa na uwezo wa kutosheleza mahitaji yake ya kibinafsi.
Waumini walisalia vinywa wazi na kuanza kumsuta wakidai alikuwa na tamaa.
Aliposikia hili, mchungaji huyo alianza kuwaomba waumini msamaha.
Kituo cha habari Tuko kiliripoti habari hii kwenye Tarehe 24 Julai 2019.