Jamaa amposa mpenziwe wakati wa hafla ya kuhitimu kwake katika chuo kikuu

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 23 July 2019.

Agne Banuskeviciute, mwanadada wa umri wa miaka 25, aliposwa na mpenziwe wakati wa hafla ya kufuzu kwake katika Chuo Kikuu cha Essex, Uingereza.

Agne alikuwa na hisia mseto kwa kuwa alijua kulikuwepo na jambo, lakini hakujua lilikuwa ni lipi.

Alisema, "Nakumbuka nikiwa jukwaani. Nilikuwa na hisia mseto kwa kuwa nilijua kulikuwepo na jambo."

Aliongeza, "Kisha kila kitu kilitendeka kwa haraka kwani ilinichukua muda kabla nibaini kilichokuwa kikifanyika."

Agne aliposwa na mpenziwe, alikuwa na furaha mara dufu, na alifichua jinsi alivyoingiwa na hofu kumwona mpenziwe akielekea jukwaani.

Wawili hao wamekuwa wakichumbiana kwa takriban miaka tisa, na wamekuwa marafiki tangu wakiwa shule ya upili.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...