Boris Johnson Chaguliwa Kuwa Waziri Mkuu Mpya wa Uingereza

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 23 July 2019.

Uchaguzi uliofanywa kwa muda wa majuma saba ulikuwa na matokeo muhimu kwa siasa za Uingereza, na Boris Johnson akashinda mpinzani wake Jeremy Hunt kwa kura 92,153 dhidi ya 46,656.

Boris Johnson, ambaye aliyechaguliwa kuwa kiongozi wa chama cha Conservative Jumanne Julai 23, atapokea wadhifa huo kutoka kwa Waziri Mkuu anayeondoka Theresa May hapo kesho Jumatano, Julai 24.

Boris Johnson ameahidi kuiunganisha nchi ambayo kwa sasa inakumbwa na mzozo wa kisiasa, na viongozi kadhaa akiwemo Rais wa Marekani Donald Trump na Theresa May tayari wamempongeza Boris kwa ushindi huo.

Habari hii inatokana na gazeti la The Guardian nchini Uingereza.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...