Malawi: Mshambulizi Hassan Kajoke apokea kuku kama zawadi kwa kuandikisha matokeo bora

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 23 July 2019.

Julai 21, 2019, siku ya Jumapili, Hassan Kajoke, mshambulizi kutoka Malawi, alikuwa mchezaji bora katika ligi dhidi ya malimbukeni Karonga United TNM.

Mechi hiyo iliyoandaliwa katika uwanja wa Kamuzu, ilishuhidiwa Nyasa Big Bullets wakiwapachika wapinzani wao mabao 5-0, huku Kajoke akiibuka kuwa mchezaji bora katika mechi hiyo.

Alitunukiwa kuku baada ya kuandikisha matokeo bora, na shabiki wake aliyemuomba ruhusa ili kumkabithi zawadi yake.

Shabiki huyo alihakakikisha kuwa kuku huyo ana rangi sawia na jezi waliokuwa wamevalia mabingwa hao wa Super Ligi.

Clubs hiyo ilianika picha ya Kajoke akipokea kuku huyo kwenye mtandao wao wa Facebook, na kuibua hisia mseto mtandaoni.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...