Skip to main content

Sonko na Passaris Wameelekea Kuridhiana Tenan

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 23 July 2019.

Sonko na Passaris Wameelekea Kuridhiana Tenan

Gavana wa Nairobi Mike Sonko na Mwakilishi wa Kike wa Kaunti hiyo Esther Passaris wameelekea kuridhiana tena baada ya kuvuana nguo hadharani Juni 1.

Waliandamana na Rais Uhuru Kenyatta katika hafla ya uzinduzi upya wa Kiwanda cha Kampuni ya Maziwa ya KCC, Mowlem, Dandora, Nairobi, Jumamosi, Julai 20.

Wakiwa kwenye uzinduzi huo, Sonko na Passaris walionekana wakishiriki mazungumzo bila ya kuoneana aibu, na mojawapo wa picha imeashiria kuwa, huenda wameridhiana hatimaye.

Wizara ya Utumishi wa Umma, Vijana na Masuala ya Jinsia ililazimia kutoa taarifa ikikashifu vikali ilichotaja kuwa mtindo mbaya wa baadhi ya viongozi kushambulia na kuwadunisha viongozi wanawake.

Wabunge wa kike wakiongozwa na Mbunge wa Suba Kaskazini Millie Odhiambo walimshutumu sana Sonko kwa kumkosea heshima Passaris.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →