Wabunge wa Magharibi Wanasema Hatawezi Mung'umi Mkono Mgomoa wa Urusi 2022

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 19 July 2019.

Wabunge wa Magharibi Wanasema Hatawezi Mung'umi Mkono Mgomoa wa Urusi 2022

Wabunge wa eneo la Magharibi mwa Kenya walisema hawatamuunga mkono mgombea yeyote wa urais ambaye hana ajenda ya maendeleo katika eneo hilo.

Wabunge hao walisema kuwa lazima kuwepo na majadiliano kwa ajili ya kuishirikisha jamii ya Waluhya kwenye serikali.

Naibu Rais William Ruto na baadhi ya wanasiasa kutoka eneo la Magharibi mwa Kenya katika hafla ya awali.

Wabunge hao walisema kuwa mgombeaji yeyote anayetaka kuungwa mkono eneo la Magharibi ni sharti ajiandae kufanya majadiliano nao kuhusu ni vipi jamii ya Waluhya itanufaika.

"Naibu Rais ni jirani yetu na rafiki lakini hataweza kupata uungwaji mkono wa moja kwa moja iwapo hapatakuwepo na majadiliano ya jinsi jamii ya Waluhya itanufaika kwa kumuunga kupata urais," Wangwe alidokeza.

Wanasiasa kutoka eneo hilo kufurika katika chama cha ANC kufuatia tangazo la Mudavadi kwamba atawania urais 2022.

Wanasiasa hao walisema kwamba wakati wa kupata rais atakayeiongoza nchi kutoka eneo la Magharibi mwa Kenya umewadia na siasa za kutumiwa na kutemwa na wagombea urais wa ameneo mengine umefika kikomo.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...