This archive report was first published on 18 July 2019.
Lydia Forson, mwigizaji wa Ghana, amesema kuwa shinikizo la kijamii ni sababu kuu ya wanawake wengi kuhatarisha maisha yao ili waweze kuwa kivutio kwa wanaume na kuwafanya wawe waaminifu katika ndoa.
Amesema hili kupitia ukurasa wake wa Twitter, na kuongeza kuwa sababu hii ni kwa sababu jamii inawaelimisha wadhamini mapenzi kuliko kitu chochote kile.
Forson amesema kuwa kila mwanamke anahisi kwamba mwanaume ni kila kitu anachokihitaji maishani, na hivyo kuwafanya wawe mbioni kutafuta mapenzi kwa vyovyote vile.
Amesema pia kuwa wengi wao wameripotiwa kutafuta mvuto wa mapenzi kutokana na shinikizo kutoka kwa wanawake wenzao.
Forson amesema hii baada ya makundi kadhaa ya wanaume kutoka Afrika Magharibi kuonekana wakiwa kwenye foleni ndani ya duka moja wakitafuta dawa za mvuto wa mapenzi na yale ya kuwazuia wanaume kuwa na wapenzi wa kando.
Amesema pia kuwa wengine walikuwa wameenda kutafuta dawa za kuwafanya wawe magwiji kitandani.