Maafisa Wa KWS Wamkamata Wafanyabiashara 15 Wenye Nyama ya Punda Milia Soko la Burma

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 29 June 2019.

Mnamo tarehe 29 Juni 2019, maafisa wa Idara ya Kuwalinda Wanyama Pori (KWS) waliwakamata wafanyabiashara 15 katika soko la Burma wakiwa na kilogramu 800 za nyama ya punda milia. Inaaminika kwamba nyama hiyo ilikuwa tayari imenza kuuziwa kwa wananchi.

Kulingana na taarifa ya KWS, maafisa hao walisema kwamba walianza kuwachunguza wafanyabiashara hao baada ya kuonekana wakiondoka na punda milia katika shamba la Portland Athi River, Machakos.

Maafisa wa KWS wakishirikiana na maafisa wa polisi walianza kuwafuata washukiwa hao ambao inaaminika wamekuwa wakishiriki uwindaji haramu. Gari lililokuwa likitumika katika usafirishaji wa nyama hiyo pia lilikamatwa.

Endapo washukiwa hao watapatikana na makosa ya uwindaji haramu na uuzaji wa nyama pori basi watafungwa jela kwa muda usiopungua miaka mitatu. Washukiwa watafikishwa mahakamani Jumamatu.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...