This archive report was first published on 29 June 2019.
Naibu Rais William Ruto amejivunia kufuzu kwa bintiye Stephanie Jepchumba katika taaluma ya uanasheria kutoka chuo kikuu cha Strathmore mnamo Juni 28, 2019. Hii ni baada ya Stephanie kuwa miongoni mwa mamia ya mahafala wengine waliohitimu shahada mbali mbali.
Alipokuwa akitoa salamu za kufuzu kwa bintiye yake, Ruto alisema kupitia ukurasa wake wa Facebook kwamba kujitolea, bidii, kujinyima kwako na neema ya Mungu vimekuwezesha kuibuka na ushindi. Pia aliwasihi wanafunzi wenzake kuzingatia haki na uaminifu katika taaluma yao.
Stephanie alifuata nyayo za ndugu yake Nick, ambaye aliteuliwa kama wakili wa mahakama kuu nchini Kenya mnamo Disemba 2018. Mwaka wa 2015, bintiye nyingine ya Ruto, Charlene, alifuzu katika taaluma ya mawasiliano kutoka chuo kikuu cha Daystar.
Wakenya mitandaoni wamempongeza Ruto kwa kuthibitisha kwamba masomo ya nchini Kenya ni ya hali ya juu. Hii imewapendeza watu wengi nchini humo, ambao wamejivunia kufuzu kwa Stephanie.
Naibu Rais Ruto alikuwa ameandamana na mkewe wakati wa hafla hiyo, na alidinda kuketi katika eneo lililotengewa wageni mashuhuri na kusisitiza kutangamana na wazazi wengine.