Shule za umma bado hazijazingatia sheria ya 2016 inayotaka serikali kujenga vituo vya kunyonyeshea watoto shuleni.
Wizara ya elimu inahitajiwa kuanzishaa vituo hivyo katika taasisi zote za umma, lakini shule za umma bado hazijazingatia sheria hiyo.
Walimu wa kike hasa walio na watoto wachanga hulazimika kwenda nyumbani mara kwa mara shule zinapofunguliwa ili kunyonyesha na hivyo kupoteza wakati na pesa.
“Tunataka kusaidia walimu wanawake walio na watoto wachanga na wanaohisi haja ya kwenda nyumbani kuwanyonyesha,” alisisitiza Benta Opande, mkurugenzi wa Muungano wa Walimu Wanawake Nchini (Kewota).