Familia ya Rubani wa DP Ruto Yadai Haki

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 14 July 2019.

Wakati wa mazishi ya rubani wa DP Ruto, Marius Magonga, familia yake ilizungumza kuhusu ajali ya ndege iliyomuua kufanya hima. Mazishi hayo yalifanyika Mabonde katika Kaunti ya Trans Nzoia Jumamosi, Julai 13.

Abdulmalik Magonga, ndugu wa rubani huyo, alisema familia hiyo ingali inasumbuliwa na ajali hiyo kwani hawajawahi kupata matokeo rasmi ya kilichofanyika na kusababisha ndege hiyo kuanguka.

Abdulmalik alisema ndugu yake alikuwa rubani mwenye tajriba na hawajaelewa ni vipi alikubali kupaa angani nyakati za usiku kinyume.

"Hatujui kilichosababisha ndege hiyo kuanguka, na kile tunaomba ni uchunguzi wa kina kufanywa na shirika la huduma za ndege nchini (KCAA). Tunahitaji matokeo kamili ili tukumbali yaliyotokea," Abdulmalik alisema.

Rubani Magonga alifariki mnamo Machi 3, 2019 wakati ndege yake ilianguka katika eneo la Lobolo Kaunti ya Turkana alipokuwa amewapeleka watalii katika kisiwa kimoja eneo jilo.

Polisi walitoa taarifa kwamba ndege hiyo ilikuwa na watu watano na wote waliangamia baada ya kuanguka mwendo wa saa mbili usiku.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...