Maaskofu wa ACK Mumias Wapiga Marufuku Mazishi ya Wikendi

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 11 July 2019.

Maaskofu wa Kanisa la Kiangilikana la diosisi ya Mumias wamepiga marufuku mazishi ya wikendi, kwa ajili ya kuwazuia wanasiasa kuingilia kati na kutatiza shughuli za mazishi.

Imeonekana kuwa hafla nyingi za mazishi zinapigwa wikendi, na wanasiasa wanapata fursa ya kupiga siasa badala ya kuacha familia zilizofiwa kuomboleza mpendwa wao.

Askofu wa kanisa hilo Joseph Wandera alisema uamuzi huo umefanywa baada ya mashauriano na watahakikisha kwamba hafla yoyote ya mazishi inafanywa siku za wiki pekee.

"Tunawatambua na tunawajali wanasiasa wetu ila ibada za mazishi zimekuwa zikiingiliwa sana na wanasiasa na kufanya zikose umuhimu, tutazidi kuwatambua wanasiasa wetu lakini hatutakubali watatize hafla zetu za mazishi," Wandera alinukuliwa na Nation.

Maaskofu hao wataendesha hafla za mazishi siku za Jumatatu hadi Ijumaa pekee.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...