Skip to main content

Machakos: Kioja Chashuhudiwa Mademu Wakipigania Sponsa

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 10 July 2019.

Kituo cha habari Tuko liliripoti kuwa kioja kilichowaacha wakaazi wa eneo la Mikuini, kaunti ya Machakos midomo wazi baada ya mwanadada kumfungia mwenzake chumbani na kumpa kichapo kwa kujaribu kumpokonya sponsa.

Allegations zinaonyesha kwamba kabla ya kisa hicho, vipusa hao walikuwa chanda na pete ila uhusiano huo ulikatika ghafla pale ambapo mwanadada aligundua mwenzake alikuwa akimvizia sponsa wake.

Alipofika mahali hapo, mwenye nyumba alidinda kumsalimia mwenzake, lakini kidosho alifunga mlango na akaanza kumtandika mwenzake huku akimlaumu kwa kujaribu kuingilia penzi lake na jamaa wake.

"Ni lazima utamkoma mpenzi wangu la si hivyo, nakuharibu sura leo leo," demu alimfokea mwenzake.

Wakati huo huo, majirani walifika mahali hapo na kumwokoa mwanadada huyo huku wakimsuta vikali.

Source: Tuko

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →