This archive report was first published on 10 July 2019.
Shabiki mkuu wa AFC Leopards Joram Akonje, ambaye alijulikana kama Bishop, amefariki. Akonje alikuwa akijitokeza katika mechi zote za Ingwe.
Alipatikana amefariki nyumbani kwake katika kaunti ya Vihiga, huku akiwa amejikita katika soko la Kima eneo la Magharibi mwa Kenya.
Aliondoka nyumbani kwake katika mtaa wa Mathare, akielekea kijijini kwao Bunyore katika kaunti ya Vihiga, lakini alipatikana amefariki katika hali ya kutatanisha.
Polisi wanachunguza kisa hicho huku mashabiki wa klabu hiyo kupitia mtandao wa jamii wakiongozwa na nahodha wa zamani Duncan Otieno, wakituma risala zao za rambi rambi kwa shabiki huyo wa kufa kupona.