Wakenya Waorodheshwa Katika Nafasi ya Pili Kwa Urembo Barani Afrika

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 9 July 2019.

Wakenya wameorodheshwa katika nafasi ya pili barani Afrika kwa urembo, kulingana na utafiti uliofanywa na shirika la Big 7. Nchi ya Afrika Kusini ilishikilia nafasi ya kwanza.

Utafiti huo ulitumia kigezo cha Lupita Nyong'o, mshindi wa tuzo la Oscar, kama kigezo cha kuwaorodhesha Wakenya katika nafasi hiyo.

Kenya iliorodheshwa katika nafasi ya kumi na nne, huku Afrika Kusini ikiishikilia nafasi ya sita kote ulimwenguni.

Ukrain ilishikilia nafasi ya kwanza katika ripoti hiyo ya Big 7, kwa sababu ya urembo na mvuto wa kipekee wa wananchi wa nchi hiyo.

Wananchi kutoka Denmark, Ufilipino, Brazil, na Australi walishikilia nafasi za pili, tatu, nne, na tano mtawalia.

Timu hiyo iliwashirikisha watu 1.5 milioni ambao walitakiwa kutoa mtazamo wao na kupiga kura kuhusiana na mdahalo huo.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...