Murkomen Under Fire for Alleging Police Mistake in Itumbi's Arrest

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 4 July 2019.

Seneta wa Elgeyo Marakwet, Kipchumba Murkomen, amekabiliwa na vikwazo vya kijamii baada ya kudai kwamba maafisa wa polisi walikosea kumkamata mkurugenzi mkuu wa mawasiliano ya kidijitali katika ikulu, Dennis Itumbi, kwa kueneza barua ghushi inayodaiwa kuwa na ujumbe wa kumuua Naibu Rais William Ruto.

Itumbi alikamatwa Jumatano Julai 3, na maafisa kutoka Idara ya Upelelezi DCI kwa kuhusishwa na barua ghushi hiyo.

Murkomen alitaka maafisa wa upelelezi kuwakamata waliohusika na barua hiyo, lakini sio mtu yeyote tu.

Alisema, "Kwa hivyo, itumbi alikatwa kwa kueneza barua ghushi kwenye kundi la WhatsApp la wanachama wa Tangatanga, ni watu wangapi wamesambaza barua hiyo?, hebu na vyombo vyote vya habari vilivyoeneza barua hiyo pia vichukuliwe hatua," Murkomen alisema kwenye mtandao wa Twitter.

Itumbi alifunguliwa mahakamani Alhamisi Julai 4, na atazuiliwa tena kwa siku tano ili uchunguzi zaidi ufanywe dhidi yake.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...