Wakenya wamshambulia Karua baada ya Safaricom kuteua Michael Joseph kama kaimu afisa mtendaji

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 2 July 2019.

Wakenya wamefupisha kiongozi wa chama cha Narc Kenya, Martha Karua, baada ya Safaricom kuteua Michael Joseph kama kaimu afisa mtendaji.

Michael Joseph aliteuliwa kushikilia wadhifu huo kufuatia kifo cha aliyekuwa afisa mtendaji Bob Collymore Jumatatu Julai 1 baada ya kuugua saratani ya damu.

Julai 1, 2019, ilikuwa siku ya kifo cha Bob Collymore, aliyekuwa afisa mtendaji wa Safaricom.

Karua alisema Safaricom ilionyesha hadharani kutokuwa na imani na wafanyakazi wake wakuu ilipoamua kumteua Joseph kama kaima afisa mkuu mtendaji.

"Hivi sio vema kabisa, inaonekana bodi ya Safaricom ilikosa imani katika wafanyakazi wake wakuu ndiposa ikaamua kumteua Michael Joseph," Karua aliandika Twitter.

Michael Joseph ni mwenyekiti wa kampuni ya Kenya Airways kwa sasa.

Joseph alihudumu kama afisa mkuu mtendaji wa kampuni hiyo kutoka mwaka wa 2000 hadi 2010 ambapo marehemu Collymore alichukua hatamu za uongozi.

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...