This archive report was first published on 2 July 2019.
Julai 1, 2019: Mbunge wa Tiaty William Kamket amemjibu vikali naibu Rais William Ruto baada ya kumuita Raila Odinga 'mfalme wa umaskini' humu nchini.
William Kamket alisema Ruto hapaswi kumtaja Raila kuwa mfalme wa umaskini ikizingatiwa kwamba mwenyewe hawezi akaepuka kuitwa mwizi mkuu.
Alisema, "Nimesikia Ruto akisema Mheshimiwa Raila Odinga ni mfalme wa umaskini, nafahamu kuwa Ruto anajua sana kuwapa watu majina ila anapaswa kujua kwamba hata mtoto mdogo akiulizwa mwizi ni nani, atakwambia ni Ruto," Kamket alisema.
Alidai umaskini utaisha hivi karibuni lakini jina mwizi litakuwepo milele.