Wanawake wazua kioja baada ya kulishana makonde hadharani wakizozania leso

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

Primary source Kenyan Digest archive

This archive report was first published on 2 July 2019.

Wanawake wawili wa Liani, Machakos, walishuhudia sisema ya bure baada ya kulishana makonde hadharani wakizozania leso.

Wanawake hao walikuwa wamehudhuria sherehe iliyoandaliwa katika eneo hilo ambayo ilikuwa ya kufana mno.

Mapambano yalienda kombo pale ambapo kikundi cha akina mama kilianza kutunukiwa zawadi za leso, na wanawake hao walianza kubishania leso moja iliyokuwa imebaki.

Uvuta nikuvute hiyo ilishuhudiwa baina ya wanake hao ambapo kila mmoja alionekana kuvuta kamba upande wake akitaka awe ndio wa kutunukiwa.

Mzozo huo ulizidi na mama mmoja akamrukia na kumzaba kofi mwenzake huku akimfokea.

"Hii leso ni yangu. Mimi ndio nimefika hapa wa kwanza. Usiniletee nyenyenye zako," mama mmoja alisikika akimwambia mwenzake.

Source: Tuko.co.ke

Next read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim Exposed Over Refusal to Repay Ksh 2 Million Debt as Protest Looms at Talanta Plaza

24 July 2026 · 4 min read

Sports Fund CEO Nuh Ibrahim has been exposed over his refusal to repay a KSh2 million debt to a young businessman, with a peaceful...