Skip to main content

Urafiki wangu na Ruto sio wa siri, mambo makubwa yako njiani - Kiunjuri ▷ Kenya News

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 30 June 2019.

Waziri wa Kilimo Mwangi Kiunjuri amesema joto la kisiasa linaloshuhudiwa humu nchini ni la kawaida. Hata madai ya kuwepo kwa njama ya kumuua Naibu Rais William Ruto ni jambo la kawaida.

Waziri huyo alisema hii wakati wa kujadiliwa na gazeti la Taifa Leo. Alisema kuwa ana urafiki na Ruto, na kuwahakikishia Wakenya kuwa watarajie mambo makubwa zaidi katika ulingo wa siasa.

Aliongeza kuwa yeye hana habari zozote kuhusu mipango ya kumuangamiza Ruto na kwamba hakuhudhuria mkutano wa mkahawa wa La Mada ambapo inadaiwa njama hiyo ilipangwa.

Alisema kuwa ana urafiki na Ruto, na kuwahakikishia Wakenya kuwa watarajie mambo makubwa zaidi katika ulingo wa siasa. Alisema kuwa ana urafiki na Ruto, na kuwahakikishia Wakenya kuwa watarajie mambo makubwa zaidi katika ulingo wa siasa.

“Huu ni msimu wa siasa; mengi yapo njiani yaja na utasikia ya kushtua, ya kuchekesha, ya kuudhi na ya kila aina. Nimekuwa kwa siasa kwa muda na ninayaelewa haya maneno,” alisema Kiunjuri.

Waziri huyo amevitaka vyombo vya dola kuhakikisha kuwa Wakenya wanafahamu ukweli kuhusu madai hayo kwa kufanya uchunguzi wa kina.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →